Skip to main content

Curriculum Vitae .... 3

Sehemu ya pili tuliona vipengele vya Education background/qualification na Work Experience, Leo tumalizie vipengele vingine muhimu katika uandaaji wa C. V.

4. Training.
Hapa unapaswa kuandika mafunzo yote ambayo umeyapitia kwa kuzingatia mwaka yaani unaanza na recent training to old. Usisahau kuandika taasisi au chama kilichotoa training hiyo.

5. Awards and Achievement
Katika sehemu hii unapaswa kuandika awards mbali mbali ambazo umewahi kutunukiwa. Inaweza kuwa shule ni, chuoni, kazini ama sehemu yoyote inayotambulika. Unapoweka award hiyo kumbuka ni lazima uwe na uthibitisho yaani cheti. Utaratibu wa uandishi ni kuanzia na recent to old.

6. Skills
Sehemu muhimu sana na huangaliwa kwa jicho pevu wakati wa kuomba kazi. Hapa utaandika stadi zako na ujuzi ulionao, mfano lugha, reading, writing, computer, administration skills na kadhalika. Kumbuka unapoandika skill usiyonayo ni hatari kwa C. V yako.

7. Membership
Katika sehemu hii unatakiwa uandike kama wewe ni member wa taasisi au organization yoyote ile. Kumbuka kuandika na cheo chako au wajibu wako.

8. Publication
Sehemu hii sio ya kila mtu, Bali ni kwa wale waandishi tu. Unatakiwa kuandika kazi mbakimbali ambazo umechapisha au hata ambazo hujachapisha yaani unpublished. Itakuongezea credit katika C. V yako.

9. Hobbies and Interests
Katika sehemu hii utaandika vile uvipendavyo kwa ufupi tu na kuvitaja. Mfao swimming, jogging, Reading, Watching TV shows etc.

10. Referee
Hapana sasa, unatakiwa kusema watu ambao wataweza kusema juu yako. Watu hao ni lazima wawe wanakufahau vizuri na unashauriwa uwe umewapa taarifa kwamba ndio referee wako. Kwa kawaida watu hao wasizidi watatu na wasipungue wawili.

               ********************

        Ushauri.... 0756775148

Popular posts from this blog

Curriculum Vitae (C. V)

Jana nilifika katika kituo kimoja cha afya na katika Harakati za hapaaaa na pale, nikiwa nimekaa kwenye benchi ili nipumzike kidogo. Nikiwa pale wakatokea wauguzi wawili nao wakakaa karibu yangu na wakaanza kuzungumza. Mmoja akamwambia mwenzake juu ya changamoto za ajira na jinsi alivyojitahidi kutafuta nafasi hata za kujitolea bila kufanikiwa, na yule mwenzake nae akamwambia jinsi alivyopambana mpaka kupata nafasi hiyo japo wanalipwa ila bado ni posho kidogo sana. Sasa, katika mazungumzo yao mwanzoni hayakunihusu japokuwa niliyasikiliza Si unajua tena sikio halina mlango lakini walifikia kipindi wakanishirikisha kwa namna moja ama nyingine hasa walipoanza kujadili vikwazo walivyokutana navyo. Ni vikwazo vingi ila hivi viwili vitakuhusu hata wewe pia. Wakisema cha kwanza ni kuandika barua ya kuomba ajira ama kujitolea na ilitakuwa iandikwe kwa lugha ya kiigereza na kingine ni kuandaa wasifu binafsi (c.v) inayoonesha mtiririko mzuri wa taarifa zako. Hapo sasa wakanishirikisha. Ngoja ...