ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA ..... Mzee Kajumba alishindwa kupambana na dhoruba Kali ili kuokoa maisha yake, hatimaye Akakata roho ,,,, je nini kitaendelea Wakati Kyle nyumbani mkewe hajui lolote ?????? ENDELEA ......... Usiku huo Bi tausi hakuwa na raha kabisa ndani ya chumba chake cha tofari za udongo ambacho kimeezekwa na nyasi. Alijaribu kutoka nje ili aone labda Mzee kajumba atakuwa amefika lakini upepo mkali haukumpa nafasi kutoka nje hivyo alijaribu kuchungulia tu wala hakuweza kuona mbele sababu ya giza kali. Akajisemea moyoni mwake ' huenda atakuwa kwa rafiki yake Bwana Juma'. Lakini haikuwa kawaida ya Mzee kajumba kuchelewa kiasi hicho jambo ambalo liliendelea kumpa wasiwasi. Aliendelea kumsubiri mme wake kipenzi mpaka usingizi ukamchukua akiwa amekaa kwenye kiti cha marimba ndani ya chumba chake . Wakati usingizi unamwachia Bi tausi ilikuwa yapata saa tisa na nusu usiku. Alipoamka hakumwona mme wake ikabidi apate hofu zaidi, bila kujali usi...