Skip to main content

Posts

Most Recent Post

NATIONAL ELECTION IN KENYA 2017

NI SALAMA KENYA. Safari iso ndefu, leo mnaitimiza Kama mbio za sakafu, ukingoni mwamaliza Chagua iloturufu, kwa Kenya yenye mwangaza Ni salama ni amani, Kenya tunaihimiza. Chaguzi ni siku moja, mchague wa moyoni Wala msilete vioja, kuivuruga amani Sote ni ndugu moja, mnachagua rubani Ni salama ni amani, Kenya tunaihimiza. Kwa sala namwomba Mungu, alotuweka duniani Wasitufitini wazungu, Afirika ina amani Uchaguzi mwema wezangu, sisi kwenu majirani Ni salama ni amani, Kenya tunaihimiza. ©UPP2017
Recent posts

'SIJINYIME

'SIJINYIME. NGELEJA©UPP Bandu na bandu kidogo, Utamu wake mkolezo Wala sinipe kisogo, Zidisha kale kamchezo N'kikugusa usiwe mbogo, Njoo upate tulizo Raha ya huba uwazi, Mfichaji ni mwibaji. Niite bebi niitike, nami nikwite laazizi Sura yako isifutike, Moyoni iweke mizizi Unonapo njoo udeke, Walozi uwanyime pumzi Raha ya huba uwazi, Mfichaji ni mwibaji Nikushike utakapo, Nilishe chakula chako Wanojisifu kwa matapo, wamalize kwa kicheko Tuvuke mito mbili popo, nishiriki raha zako Raha ya huba ni wazi, Mfichaji ni mwibaji.

UCHAGUZI WA RAIS RWANDA AUGUSTI 4

KILA LA HERI RWANDA. NGELEJA©UPP Uchaguzi umewadia, Raisi kumchagua Agusti nne historia, Rwanda imeshatimia Amani tulojiwekea, Ni vyema kuilinda pia Sote ni ndugu raia, Na nchi imetulia Kila kheri nawaombea, Na chaguo jema pia.

EMPTY HANDS

EMPTY HANDS by Ngeleja© upp Solemn echo Shaken my arms Too much twinkle Troubles my days Struggles be for Yield but no fruits How far to be so Should achieve my grants

THE KILLER

KILLER. NGELEJA©UPP Black mask  Bloody teeth The vampire Defeat activists Revamp superiority Illuminated By devilish Many scream From homeless Hopeless no helpfulness Wandering left to right Eating mushroom Gifting nuts Celebrating mourns Families depart Going to war Healing their backs Pain nervously Dare not near Killer Muller Better Amini Dada Than Killer Murder.

AT 25 YEARS

LEO NAOMBA TUSHIRIKI JAMBO HILI: Duniani kote miaka hii ya 2000 vijana tumekumbwa na changamoto kadha wa kadha. Mfano Ajila, Elimu na hata Malazi na Magonjwa (kwa kutaja chache). Hali hii imepelekea wengi kukosa muelekeo sahihi wa maisha na hata ndogo za wengi kufutikia gizani. Kama kijana, yapo mambo mengi ambayo unapaswa kuyakamilisha au wakati mwingine kuwa nayo kabla umri ya ujana haujakuacha. Kumbuka siku zinasogea kwa kasi sana. Jiulize tuu hapo ulipo una miaka mingapi na baada ya miaka 5 ijayo utakua na mingapi. Hivyo basi zote ni changamoto ambazo tunapitia na tunatakiwa kuzishinda. Pamoja na suala la elimu (ambalo si lazima sana) kijana unatakiwa kufanya yafuatayo kabla hujamalikisha miaka 25. Ni mambo matatu tu: 1. Uwe umeshawahi kufanya biashara: hapa haijalishi kama bado inaendelea au ulifanya biashara kisha mtaji na faida vikaporomoka. Kikubwa uwe umeshawahi kufanya biashara yako binafsi. Hii itakuwa imekusaidia kujua changamoto ambazo zipo katika biashara mapeeeema uk...

ETI KISA UMEUMBIKA!!

ETI KISA UMEUMBIKA! NGELEJA©UPP Rabi sinipe mapenzi, sijapata wa kuyaenzi Bora n'zidishie tenzi, neleze hizi simanzi Liko wapi lile penzi, uloapa utalienzi Namba nane yako figa, moyoni mwangu ni mwiba. Sote tulitii kiapo, maisha yangu ni yako Hata popote tuendapo, u mlinzi nami ni wako Hani ulipo mi nipo, ilikua ahadi yako Namba nane yako figa, moyoni mwangu ni mwiba Miezi kenda yapita, mke hujanipa tunda Ndani warudi saa sita, hii tabia yanishinda N'kihoji wakunja ndita, eti mi si wa kukulinda Namba nane yako figa, moyoni mwangu ni mwiba Unapenda vitu ghari, pesa magari swadakta Unasema we mzuri, vigogo wengi wadata Wajipuliza uturi, na waenda kula bata Namba nane yako figa, moyoni mwangu ni mwiba Pombe wanywa nyakanyaka, nusu uchi wavaa Mwili watoa sadaka, wala huogopi zinaa Sio mabosi si vilaka, wote umewapa ridhaa Namba nane yako figa, moyoni mwangu ni mwiba. Wamekuhonga na gali, sasa na ndani hulali Ndoa wachezea kamali, Kwa mora dua nasali Kama sik...

NIKIMPATA

NIKIMPATA NGELEJA©UPP Mahaba anifundishe, nami nimuelimishe Furaha airejeshe, kwa huba nimleweshe Asijeleta kasheshe, kunonjesha sitosheke Nakutunzia heshima, tufurahi nikikupata Kwa uchesi nisemeshe, huku ukitabasamu Hata chakula unilishe, muda wote nipate hamu Nibebe usinishushe, wenye wivu wajilaumu Nakutunzia heshima, tufurahi nikikupata Nimdekeze kwa dhati, nitamwimbia na nyimbo Kwangu itakua bahati, kama akiunasa ulimbo Niwe shati yeye koti, asiniletee misimbo Nakutunzia heshima, tufurahi nikikupata Moyo ushafunguka, njoo uingie nifunge Wala usijezunguka, kwa Wengine wakusonge Njoo kula kinacholika, kataa wasikuhonge Nakutunzia heshima, tufurahi nikikupata. Contact: 0756775148

LIFE MAKER

LIFE MAKER By NGELEJA©UPP Dream comes forth times Flashes upon my eyes fresh What next. Last episodes Majorities satisfied Streets no foes nor notorious Before The Male Fox life was Sweet I dream money in hard time Vacancies minorities’ fear "We enough" their slogan My degree is a grave pot Would we yell like Canaanites? Asks multitudes Trading brings no values VAT highest, Politics colonize economics Work! Work! Work! For National benefits. "We leaders" their slogan. Remember what you told us in first feast “You are a Lion but never eat meat” Now, who to enjoy hidden meat Or "Akiba haiozi" you will enjoy after feast? Ngeleja©upp 0756775148

NITAKUMBUKWA KWA KIPI?

NITAKUMBUKWA KWA KIPI? NGELEJA©UPP. Kwa pesa au majumba ya kifahari mujini Ama kumiliki shamba na ng'ombe wengi kijijini Vipi kwa yangu kasumba kugawia pesa masikini Swali lautesa moyo NITAKUMBUKWA KWA KIPI? Nimejaaliwa ucheshi je itakua kumbukizi? Au kwa wangu ubishi fujo na hasira za mkizi Uchoyo huwa sikopeshi na kiduchu kauwizi Swali lautesa moyo NITAKUMBUKWA KWA KIPI? Je ni bora uongozi au uongozi bora Kwa uzuri wa malezi ama kwa wingi ukora Au ni uzuri wa mavazi na uanamitindo bora Swali lautesa moyo NITAKUMBUKWA KWA KIPI? Sura yenye mvuto maulana kanijalia Utanashati wa Vito na shepu ya kuvutia Je kutembea kwa mnato na sauti inayovutia Swali lautesa moyo NITAKUMBUKWA KWA KIPI? Kwa salamu maridhawa ambazo nakutumia Au msaada wa ile dawa wakati umeugua Je utaona sawa kunikumbuka kwa umbea? Swali lautesa moyo NITAKUMBUKWA KWA KIPI? Ukimya nilouweka miaka hatujaonana Siku sasa umezeeka je ndo tanikumbuka sana? Umaarufu niloweka mitandaoni napatikana Swal...

NJOO NAE TUFURAHI

NJOO NAE TUFURAHI. Kwanza nawapa salamu, baba na mama pokeeni Kwa bashasha na hii hamu, kaka na dada hongereni Kwa kuhitimisha kaumu, watunzi wote poleni Vizuri usile pekeako, njoo nae tufurahi Vizuri usile pekeako, njoo nae tufurahi Sasa hili kundi ni lako, litumie kwa usahihi Itume hadithi yako, Wimbo, shairi hata futuhi Vizuri usile kepeako, njoo nae tufurahi Njoo uimbe usome, njoo ucheke uburudike Kwa tungo zisizo ukame, njoo ujifunze uadilike Huu wigo wote tuungame, tulipokosa tuimarike Vizuri usile pekeako, njoo nae tufurahi Kazi kwako ni moja, itimize usipuuze Ili tuongeze hoja, rafikizo uwaongeze Wajaze kwa kundi moja, wote kisha tuwapongeze Vizuri usile pekeako, njoo nae tufurahi Writer: baraka ngeleja 0756775148

MAUMIVU

MAUMIVU Sili wala silali, ninakesha kama bundi Umenichoma msumari, haoung'oki hata kwa fundi Najua waona fahari, vicheko vyakutoka sundi Maumivu ndo jina langu, nipe pole salamu yangu Moyo wangu bado una jambo, nisikize mpenzi wangu Kwako nishanasha chambo, usisulubu mtima wangu Wengi wamekupa ulimbo, wakunase UA langu Maumivu ndo jina langu, nipe pole salamu yangu. Mangapi niliyapuuza, yalosemwa juu yako Leo mambo wayakuza, eti mie sio taipu yako Na vita unaitangaza, ama zangu ama zako Maumivu ndo jina langu, nipe pole salamu yangu. Kupenda hisani ya moyo, usiniumize mwenzio Hata fukara haki ninayo, rudi unitulize mwenzio Wakupao pesa wachoyo, wa penzi zaidi ya kileo Maumivu ndo jina langu, nipe pole salamu yangu Nauguza kidonda changu, unanitesa mpenzi wangu Hakuna raha tena kwangu, ebu tazama machozi yangu Vingi ulinizoesha wangu, chonde rudi hima kwangu Maumivu ndo jina langu, nipe pole salamu yangu. Ona watoto wanalia, subira imewaishia Majirani walokuzoe...

HATIMAYE AMEOLEWA

HATIMAYE AMEOLEWA. Kwa miaka zaidi ya kenda, urafiki tuliukoleza Japo mbali nikaenda, pesa kuitafuta Muheza Mupenzi alijilinda, nami penzi nikatunza Leo nalia mwenyewe, hatimaye ameolewa Ahadi tulitukuza, penzi tusije livunja Maneno yake yalinikuza, kama samaki alinikunja Moyo huba alinuiza, Muheza buzi sikuonja Leo nalia mwenyewe, hatimaye ameolewa Simu na jumbe mahabuba, zilinipata si haba Hata sikuwaza suluba, kwa kazi zilizonikaba Nami moyo ulinijaba, nikamwekeza hadi baba Leo nalia mwenyewe, hatimaye ameolewa. Mara wiki ikakatika, mupenzi hapatikani Moyo nikajipa rika, labda simu matatani Hata mwezi ukavunjika, Sina taarifa abadani Leo nalia mwenyewe, hatimaye ameolewa Nikafuata ushauri, kwa wahenga mashuhuri Nipate vipi saburi, wa moyo sinaye habari Baba kasema ni nzuri, kama nikipanga safari Leo nalia mwenyewe, hatimaye ameolewa Mwaka ulofata julai, nikarudi Shambarai Huku najipa tumai, nenda posa wangu Nai Furaha isiyokinai, kwa moyo wangu jinai Leo nali...

FURSA KWA WAANDISHI WA KAZI ZA FASIHI

Fursa.

Check out @barakanichoraus's Tweet: https://twitter.com/barakanichoraus/status/858917126060552192?s=09