Skip to main content

'SIJINYIME

'SIJINYIME.
NGELEJA©UPP

Bandu na bandu kidogo, Utamu wake mkolezo
Wala sinipe kisogo, Zidisha kale kamchezo
N'kikugusa usiwe mbogo, Njoo upate tulizo
Raha ya huba uwazi, Mfichaji ni mwibaji.

Niite bebi niitike, nami nikwite laazizi
Sura yako isifutike, Moyoni iweke mizizi
Unonapo njoo udeke, Walozi uwanyime pumzi
Raha ya huba uwazi, Mfichaji ni mwibaji

Nikushike utakapo, Nilishe chakula chako
Wanojisifu kwa matapo, wamalize kwa kicheko
Tuvuke mito mbili popo, nishiriki raha zako
Raha ya huba ni wazi, Mfichaji ni mwibaji.

Popular posts from this blog

Curriculum Vitae (C. V)

Jana nilifika katika kituo kimoja cha afya na katika Harakati za hapaaaa na pale, nikiwa nimekaa kwenye benchi ili nipumzike kidogo. Nikiwa pale wakatokea wauguzi wawili nao wakakaa karibu yangu na wakaanza kuzungumza. Mmoja akamwambia mwenzake juu ya changamoto za ajira na jinsi alivyojitahidi kutafuta nafasi hata za kujitolea bila kufanikiwa, na yule mwenzake nae akamwambia jinsi alivyopambana mpaka kupata nafasi hiyo japo wanalipwa ila bado ni posho kidogo sana. Sasa, katika mazungumzo yao mwanzoni hayakunihusu japokuwa niliyasikiliza Si unajua tena sikio halina mlango lakini walifikia kipindi wakanishirikisha kwa namna moja ama nyingine hasa walipoanza kujadili vikwazo walivyokutana navyo. Ni vikwazo vingi ila hivi viwili vitakuhusu hata wewe pia. Wakisema cha kwanza ni kuandika barua ya kuomba ajira ama kujitolea na ilitakuwa iandikwe kwa lugha ya kiigereza na kingine ni kuandaa wasifu binafsi (c.v) inayoonesha mtiririko mzuri wa taarifa zako. Hapo sasa wakanishirikisha. Ngoja ...