Skip to main content

MAUMIVU

MAUMIVU
Sili wala silali, ninakesha kama bundi
Umenichoma msumari, haoung'oki hata kwa fundi
Najua waona fahari, vicheko vyakutoka sundi
Maumivu ndo jina langu, nipe pole salamu yangu

Moyo wangu bado una jambo, nisikize mpenzi wangu
Kwako nishanasha chambo, usisulubu mtima wangu
Wengi wamekupa ulimbo, wakunase UA langu
Maumivu ndo jina langu, nipe pole salamu yangu.

Mangapi niliyapuuza, yalosemwa juu yako
Leo mambo wayakuza, eti mie sio taipu yako
Na vita unaitangaza, ama zangu ama zako
Maumivu ndo jina langu, nipe pole salamu yangu.

Kupenda hisani ya moyo, usiniumize mwenzio
Hata fukara haki ninayo, rudi unitulize mwenzio
Wakupao pesa wachoyo, wa penzi zaidi ya kileo
Maumivu ndo jina langu, nipe pole salamu yangu

Nauguza kidonda changu, unanitesa mpenzi wangu
Hakuna raha tena kwangu, ebu tazama machozi yangu
Vingi ulinizoesha wangu, chonde rudi hima kwangu
Maumivu ndo jina langu, nipe pole salamu yangu.

Ona watoto wanalia, subira imewaishia
Majirani walokuzoea, kutwa kuniulizia
Hivi kweli umeamua, pesa chanzo ukakimbia
Maumivu ndo jina langu, nipe pole salamu yangu.

Moyo umejaa imani, utarejea kwangu mpenzi
Tamaa zisikurubuni, U mbali nani ntamuenzi?
Pesa na vyote duniani, ni baraka za Mwenyezi.
Maumivu ndo jina langu, nipe pole salamu yangu.

Writer: baraka ngeleja
0756775148
Date: 16 July 2017.

Popular posts from this blog

Curriculum Vitae (C. V)

Jana nilifika katika kituo kimoja cha afya na katika Harakati za hapaaaa na pale, nikiwa nimekaa kwenye benchi ili nipumzike kidogo. Nikiwa pale wakatokea wauguzi wawili nao wakakaa karibu yangu na wakaanza kuzungumza. Mmoja akamwambia mwenzake juu ya changamoto za ajira na jinsi alivyojitahidi kutafuta nafasi hata za kujitolea bila kufanikiwa, na yule mwenzake nae akamwambia jinsi alivyopambana mpaka kupata nafasi hiyo japo wanalipwa ila bado ni posho kidogo sana. Sasa, katika mazungumzo yao mwanzoni hayakunihusu japokuwa niliyasikiliza Si unajua tena sikio halina mlango lakini walifikia kipindi wakanishirikisha kwa namna moja ama nyingine hasa walipoanza kujadili vikwazo walivyokutana navyo. Ni vikwazo vingi ila hivi viwili vitakuhusu hata wewe pia. Wakisema cha kwanza ni kuandika barua ya kuomba ajira ama kujitolea na ilitakuwa iandikwe kwa lugha ya kiigereza na kingine ni kuandaa wasifu binafsi (c.v) inayoonesha mtiririko mzuri wa taarifa zako. Hapo sasa wakanishirikisha. Ngoja ...