Skip to main content

NITAKUMBUKWA KWA KIPI?

NITAKUMBUKWA KWA KIPI?
NGELEJA©UPP.
Kwa pesa au majumba ya kifahari mujini
Ama kumiliki shamba na ng'ombe wengi kijijini
Vipi kwa yangu kasumba kugawia pesa masikini
Swali lautesa moyo NITAKUMBUKWA KWA KIPI?

Nimejaaliwa ucheshi je itakua kumbukizi?
Au kwa wangu ubishi fujo na hasira za mkizi
Uchoyo huwa sikopeshi na kiduchu kauwizi
Swali lautesa moyo NITAKUMBUKWA KWA KIPI?

Je ni bora uongozi au uongozi bora
Kwa uzuri wa malezi ama kwa wingi ukora
Au ni uzuri wa mavazi na uanamitindo bora
Swali lautesa moyo NITAKUMBUKWA KWA KIPI?

Sura yenye mvuto maulana kanijalia
Utanashati wa Vito na shepu ya kuvutia
Je kutembea kwa mnato na sauti inayovutia
Swali lautesa moyo NITAKUMBUKWA KWA KIPI?

Kwa salamu maridhawa ambazo nakutumia
Au msaada wa ile dawa wakati umeugua
Je utaona sawa kunikumbuka kwa umbea?
Swali lautesa moyo NITAKUMBUKWA KWA KIPI?

Ukimya nilouweka miaka hatujaonana
Siku sasa umezeeka je ndo tanikumbuka sana?
Umaarufu niloweka mitandaoni napatikana
Swali lautesa moyo NITAKUMBUKWA KWA KIPI?

Kwa wingi wawafuasi siku ya mazishi yangu
Au kwa kuongoza kuasi rafiki jamaa na ndugu
Kweli napata wasiwasi kipi ni kukumbukwa kwangu
Mora nijalie mema ili kwa mwema nikumbukwe.

Ngeleja©upp
0756775148

Popular posts from this blog

Curriculum Vitae (C. V)

Jana nilifika katika kituo kimoja cha afya na katika Harakati za hapaaaa na pale, nikiwa nimekaa kwenye benchi ili nipumzike kidogo. Nikiwa pale wakatokea wauguzi wawili nao wakakaa karibu yangu na wakaanza kuzungumza. Mmoja akamwambia mwenzake juu ya changamoto za ajira na jinsi alivyojitahidi kutafuta nafasi hata za kujitolea bila kufanikiwa, na yule mwenzake nae akamwambia jinsi alivyopambana mpaka kupata nafasi hiyo japo wanalipwa ila bado ni posho kidogo sana. Sasa, katika mazungumzo yao mwanzoni hayakunihusu japokuwa niliyasikiliza Si unajua tena sikio halina mlango lakini walifikia kipindi wakanishirikisha kwa namna moja ama nyingine hasa walipoanza kujadili vikwazo walivyokutana navyo. Ni vikwazo vingi ila hivi viwili vitakuhusu hata wewe pia. Wakisema cha kwanza ni kuandika barua ya kuomba ajira ama kujitolea na ilitakuwa iandikwe kwa lugha ya kiigereza na kingine ni kuandaa wasifu binafsi (c.v) inayoonesha mtiririko mzuri wa taarifa zako. Hapo sasa wakanishirikisha. Ngoja ...