Skip to main content

NATIONAL ELECTION IN KENYA 2017

NI SALAMA KENYA.

Safari iso ndefu, leo mnaitimiza
Kama mbio za sakafu, ukingoni mwamaliza
Chagua iloturufu, kwa Kenya yenye mwangaza
Ni salama ni amani, Kenya tunaihimiza.

Chaguzi ni siku moja, mchague wa moyoni
Wala msilete vioja, kuivuruga amani
Sote ni ndugu moja, mnachagua rubani
Ni salama ni amani, Kenya tunaihimiza.

Kwa sala namwomba Mungu, alotuweka duniani
Wasitufitini wazungu, Afirika ina amani
Uchaguzi mwema wezangu, sisi kwenu majirani
Ni salama ni amani, Kenya tunaihimiza.

©UPP2017

Popular posts from this blog

Curriculum Vitae (C. V)

Jana nilifika katika kituo kimoja cha afya na katika Harakati za hapaaaa na pale, nikiwa nimekaa kwenye benchi ili nipumzike kidogo. Nikiwa pale wakatokea wauguzi wawili nao wakakaa karibu yangu na wakaanza kuzungumza. Mmoja akamwambia mwenzake juu ya changamoto za ajira na jinsi alivyojitahidi kutafuta nafasi hata za kujitolea bila kufanikiwa, na yule mwenzake nae akamwambia jinsi alivyopambana mpaka kupata nafasi hiyo japo wanalipwa ila bado ni posho kidogo sana. Sasa, katika mazungumzo yao mwanzoni hayakunihusu japokuwa niliyasikiliza Si unajua tena sikio halina mlango lakini walifikia kipindi wakanishirikisha kwa namna moja ama nyingine hasa walipoanza kujadili vikwazo walivyokutana navyo. Ni vikwazo vingi ila hivi viwili vitakuhusu hata wewe pia. Wakisema cha kwanza ni kuandika barua ya kuomba ajira ama kujitolea na ilitakuwa iandikwe kwa lugha ya kiigereza na kingine ni kuandaa wasifu binafsi (c.v) inayoonesha mtiririko mzuri wa taarifa zako. Hapo sasa wakanishirikisha. Ngoja ...