Skip to main content

SAUTI KILINGENI

         SAUTI KILINGENI

Baba na mama nawajia sikilizeni
Wambie wanao pia "tulieni"
KILINGENI sio mbali sana
Tazama ile taa inawaka
Punde si punde sote
Tutaisikia sauti kama usikiavyo mauti
Ikimjia aliyestahili

Sio sauti ya vinanda ama shangwe
Sio Sauti ya vifijo ama nderemo
Sio Sauti ya vigelegele ama ngomezi
Sio Sauti za mfu ama mtu hai
Ni Sauti za kelele
Kelele zilizozaa kelele za kale
Waliochoshwa na ndwele za wakwele
Waliojeruhiwa mwili mzima kwa mawe

Ni Sauti zenye mpangilio wa haki
Iliyogandamizwa na hao vigogo
Wanaojiita wenye nazo
Kutwa nzima kuwashurutisha wasonazo
Wakiiba hisa na hisani zao
Wakila wakashiba ndipo nao walemo
Mabaki walobakizwa
Sauti ya KILINGENI isikieni

Hii Sauti sio huru nitumeni
Imepita mingi bonde na mabondeni
Vilindi na vikwazoni
Msoweza kusikia isomeni

Kote harufu ya zamu tena ni damu mbichi
Walokufa ni haramu ila ni wananchi
Tena huzikwa bila karamu mbali na nchi
Ole atoaye chozi hatodumu
Ole ulizaye chanzo utapewa sumu
Sauti inatafutwa ili mbali kufutwa
Hata fadhira nilizokupa Leo unanitupa?
Msalia mtume hakosi ibadani
Ila mla nyama mpaka umchune ndo ataacha kisilani.

                +255756775149

Popular posts from this blog

Curriculum Vitae (C. V)

Jana nilifika katika kituo kimoja cha afya na katika Harakati za hapaaaa na pale, nikiwa nimekaa kwenye benchi ili nipumzike kidogo. Nikiwa pale wakatokea wauguzi wawili nao wakakaa karibu yangu na wakaanza kuzungumza. Mmoja akamwambia mwenzake juu ya changamoto za ajira na jinsi alivyojitahidi kutafuta nafasi hata za kujitolea bila kufanikiwa, na yule mwenzake nae akamwambia jinsi alivyopambana mpaka kupata nafasi hiyo japo wanalipwa ila bado ni posho kidogo sana. Sasa, katika mazungumzo yao mwanzoni hayakunihusu japokuwa niliyasikiliza Si unajua tena sikio halina mlango lakini walifikia kipindi wakanishirikisha kwa namna moja ama nyingine hasa walipoanza kujadili vikwazo walivyokutana navyo. Ni vikwazo vingi ila hivi viwili vitakuhusu hata wewe pia. Wakisema cha kwanza ni kuandika barua ya kuomba ajira ama kujitolea na ilitakuwa iandikwe kwa lugha ya kiigereza na kingine ni kuandaa wasifu binafsi (c.v) inayoonesha mtiririko mzuri wa taarifa zako. Hapo sasa wakanishirikisha. Ngoja ...